Midahalo Mashuleni kwa Mfumo wa Bunge

YPM Yaendelea Kutoa Mafunzo kwa Walimu Kuhusu Mfumo Mpya wa Midahalo wa Parliament Debate Format (PDF)

Katika kuhakikisha walimu wa shule za sekondari wanapata uelewa zaidi juu ya mfumo mpya wa uendeshaji wa midahalo ujulikanao kama Parliament Debate Format (PDF), Youth Peacemakers Tanzania (YPM) inaendelea kutoa mafunzo maalum kwa walimu kutoka shule mbalimbali za sekondari katika Wilaya ya Lushoto. Lengo la mafunzo haya ni kuhakikisha wanafunzi wanatumia mfumo huu unaolenga kuwajengea uwezo wa kujenga hoja, kutetea mada, na kukuza ujasiri wa kuzungumza mbele ya hadhira.

Mafunzo hayo yamehudhuriwa na walimu kutoka shule za sekondari za Shambalai, Prince Claus, Magamba, Shekilindi, Kitala, Kwembago, Gologolo, Lushoto, Ubiri, Mlongwema na Migambo, pamoja na mwakilishi wa Mwenyekiti wa Maafisa Elimu Kata za Wilaya ya Lushoto, Bw. Valentino M. Hizza.

Baada ya mafunzo hayo, walimu kwa kushirikiana na YPM wameandaa ratiba maalum ya mashindano ya midahalo (debates) kwa wanafunzi, ikiwa ni hatua ya utekelezaji wa mfumo huo mpya wa PDF. Kupitia ratiba hiyo, wanafunzi watapata fursa ya kutumia ujuzi waliopata darasani katika mijadala ya kitaaluma na kijamii, ikiwemo kujifunza kuheshimu mitazamo tofauti na kujenga hoja zenye mashiko.

YPM inaamini kuwa mfumo huu wa Parliament Debate Format (PDF) utachangia kwa kiasi kikubwa katika kuboresha uwezo wa wanafunzi wa kufikiri kwa kina, kujieleza kwa ufasaha, na kushiriki kikamilifu katika mijadala yenye tija kwa maendeleo yao na jamii kwa ujumla.

YPM Unveils the Youth Advisory Committee (YAC/YAB) A Platform for Youth Voices.

The Youth Advisory Committee (YAC) / Youth Advisory Board (YAB) is an initiative established by Youth Peacemakers Tanzania (YPM) to amplify the voices of young
people in decision-making processes. The committee provides a platform where youth can share their ideas, concerns, and solutions on issues affecting their communities, ensuring that their perspectives are meaningfully included in YPM’s programs and strategies.


The YAC/YAB serves as a bridge between young people and YPM leadership, promoting inclusive participation, transparency, and accountability in organizational initiatives. Members of the committee are drawn from diverse backgrounds to reflect the realities of young people across Tanzania, with representation from different regions, genders, and
social groups.

The YAC/YAB is not only a consultative board but also a driving force for transformation, ensuring that YPM remains rooted in the priorities and aspirations of the young people it serves.

Why YAC/YAB

A platform for Youth Voice
Youth members share their lived experiences, ideas and concern.
They advise on policies, programs and strategies affecting young people

A Collaborative Body
Works in partnership with adults and leadership teams.
Members help co-create not just critique organizational strategies or campaigns.

A leadership Development Space

Offers training mentorship and real-world experience
Helps young people grow as leaders, advocates and decision makers

A Feedback Loop
Helps organization tailor services, communication and outreach to youth needs.
Encourage continous improvement through youth-centered feedback

Focus of YAB
Shaping youth programs or services
Evaluating Campaigns for Youth audiences
Informing public policy on education, health, climate, etc
Advocating for youth rights
Bridging the gap between youth and adults in institutions

YPM REPRESENTED IN NATIONAL YOUTH MEDIA ADVOCACY WORKSHOP

Youth Peacemakers Tanzania (YPM) is proud to be represented at the official launch of a new cohort under the Youth in Action Program, alongside the Media Advocacy Initiative by Ms. Salha Daniel Themed:“Empowering Youth Voices for Constructive Civic Engagement”

The workshop, organized by GNRC, brought together 20 dynamic young leaders from Dar es Salaam, Tanga, Mtwara, and Zanzibar. One of the keynote speakers was @imani.luvanga , a renowned digital influencer, who shared powerful insights on how young people can leverage digital spaces to influence change and drive positive civic engagement.

During the workshop, youth leaders had the opportunity to:✅ Strengthen leadership and civic engagement skills✅ Learn practical tools such as storytelling, mobile photography, and social media for advocacy✅ Collaborate in creating community-focused media messages✅ Join a vibrant youth network for continuous support and collective actionAt YPM, we remain committed to empowering youth with the right skills and platforms to amplify their voices, shape narratives, and build peaceful, inclusive communities.#ILeadPeace#YouthInAction@arigatou_ecp@gnrctanzania#YouthVoices #CivicEngagement #MediaAdvocacy #YouthInAction #YPMTanzania #ILeadPeace #YouthInAction

YPM Yaendesha Mafunzo ya Public Debate Format (PDF) kwa Walimu na Wakuu wa Shule Lushoto

Youth Peacemakers Tanzania (YPM), kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo wakiwemo Wakuu wa shule na Walimu wa midahalo (debate) kutoka shule mbalimbali za sekondari wilayani Lushoto, wameendesha mafunzo maalum ya Uendeshaji wa Midahalo kwa njia ya kisasa inayojulikana kama Public Debate Format (PDF).

Mafunzo haya yamehusisha shule za Shambalai, Mlongwema, Ngulwi, Prince Claus, Magamba, Ubiri, Lushoto, Kitala, Kwemashai, pamoja na Migambo. Lengo kuu la mafunzo haya ni kuwajengea uwezo walimu na viongozi wa shule ili waweze kuwawezesha wanafunzi wao kushiriki mijadala ya kitaaluma kwa namna yenye tija, uhuru wa hoja, nidhamu ya kisomi, na uwezo wa kupambanua changamoto za kijamii na kitaifa kwa kutumia hoja zenye ushahidi.

Kupitia Public Debate Format (PDF), YPM inalenga kuimarisha ujuzi wa vijana katika mawasiliano, uongozi, kufikiri kwa kina, na kushiriki katika mijadala ya kisera. Mafunzo haya ni sehemu ya mkakati mpana wa kuhamasisha ushiriki wa vijana katika utengamano wa jamii, utatuzi wa migogoro, na kukuza demokrasia shuleni.

YPM inaamini kuwa uwekezaji katika midahalo ni uwekezaji katika kizazi cha viongozi wa kesho — vijana wanaoweza kueleza, kusikiliza, na kushawishi kwa njia ya amani na mantiki.

YPM Washiriki Warsha ya Kampeni Kimaendeleo za Vyombo vya Habari Jijini Dar es Salaam

Youth Peacemakers Tanzania (YPM) iliwakilishwa na Afisa wa Mazingira na Michezo, Bw. Francis Kamote pamoja na Salha Daniel, katika warsha ya kampeni za vyombo vya habari iliyoandaliwa na CEFA Tanzania jijini Dar es Salaam.

Warsha hiyo imelenga kujenga uwezo kwa taasisi na vijana kuhusu namna ya kuendesha kampeni zenye ushawishi kupitia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii, kwa lengo la kuleta mabadiliko chanya katika jamii.

“Ni nafasi nzuri kwa vijana kama sisi kujifunza mbinu bora za kuifikia jamii kwa ujumbe wa maendeleo na uhamasishaji wenye kuleta manufaa katika nchi. Uwezeshaji huu umetufungua macho zaidi juu ya nguvu ya mawasiliano,” alisema Bw. Kamote.

YPM inaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali katika kuhamasisha maendeleo endelevu kupitia sauti za vijana.

YPM Participates in Media Campaign Workshop in Dar es Salaam

Youth Peacemakers Tanzania (YPM) was represented by Mr. Francis Kamote, the Environment and Sports Officer and Salha Daniel at a media campaign workshop organized by CEFA Tanzania in Dar es Salaam.

The workshop aimed to strengthen the capacity of organizations and youth in designing and delivering impactful media and social media campaigns to drive positive change in their communities.

“This was a great opportunity for young people like us to learn effective ways to reach the community with messages of development . This training opened our eyes to the power of communication,” said Mr. Kamote.

YPM remains committed to working with partners to promote sustainable development through the voices of young people.

Ufuatiliaji wa Maendeleo ya Vikundi vya SIG – Shume na Mziaghembei

Bw. Peter Jally, Meneja wa Miradi kutoka YPM, alifanya ziara ya ufuatiliaji na tathmini katika vijiji vya Shume na Mziaghembei kama sehemu ya juhudi za kuimarisha uendelevu wa vikundi vya vijana na wanawake vinavyosimamiwa na taasisi ya YPM.

Katika ziara hiyo, Bw. Jally alikutana na wanachama wa vikundi vya utoaji wa huduma ndogo za kifedha (SIG – Savings and Investment Groups), ambapo alifuatilia maendeleo yao, changamoto wanazokutana nazo, na kuwasisitiza kufuatilia mchakato wa usajili rasmi wa vikundi hivyo.

Aidha, alitoa elimu ya ujasiriamali pamoja na ushauri wa kitaalamu kuhusu usimamizi bora wa vikundi, ikiwa ni pamoja na utunzaji sahihi wa kumbukumbu na kuhakikisha uwazi katika shughuli zote za vikundi. Pia, aliongoza majadiliano ya pamoja kwa lengo la kutatua changamoto zinazojitokeza ndani ya vikundi hivyo.

Monitoring the Progress of SIG Groups – Shume and Mziaghembei

Mr. Peter Jally, the Project Manager at YPM, conducted a monitoring and evaluation visit in the areas of Shume and Mziaghembei as part of ongoing efforts to strengthen the sustainability of youth and women groups supported by the YPM organization.

During the visit, Mr. Jally met with members of Savings and Investment Groups (SIGs) to assess their progress, understand the challenges they are facing, and emphasized the importance of following up on the formal registration process of these groups.

In addition, Mr. Peter Jally provided entrepreneurship education and professional advice on effective group management, including proper record-keeping and ensuring transparency in all group activities. He also facilitated collective discussions aimed at addressing and resolving challenges arising within the groups.

YPM at the Gamification & Design Thinking Workshop – Nairobi, Kenya

From May 19th to 29th, 2025, Youth Peacemakers Tanzania (YPM) was honored to be represented at a powerful regional workshop on Gamification and Design Thinking, hosted by AAYMCA in Nairobi.

This dynamic initiative brought together passionate youth leaders and innovators from across Africa to explore how games and creative thinking can build better, more inclusive societies. The workshop was more than learning—it was an experience in co-creation, collaboration, and community transformation.

YPM was proudly represented by Mr. Francis Kamote – Environment and Sports for Development Program Officer, Yasin Juma and Salha Daniel Youth Representative gh hands-on sessions and collaborative challenges, the team engaged with cutting-edge tools and strategies to design game-based solutions to social issues. We’re excited to bring these insights back home and continue driving positive change through play. 🕹️💡

YPM katika Warsha ya Gamification na Design Thinking – Nairobi, Kenya 🇰🇪

Kuanzia Mei 19 hadi 29, 2025, Youth Peacemakers Tanzania (YPM) ilishiriki katika warsha ya kikanda kuhusu Gamification na Design Thinking iliyofanyika Nairobi, Kenya na kuandaliwa na AAYMCA.

Warsha hii ilikusanya vijana kutoka nchi mbalimbali za Afrika ili kujifunza jinsi ya kutumia michezo na ubunifu kutatua changamoto za kijamii na kuleta mabadiliko katika jamii zao. Warsha hii haikuwa ya kujifunza tu, bali pia ya kushirikiana, kubuni na kujenga jamii bora kwa pamoja.

YPM iliwakilishwa na Bw. Francis Kamote – Afisa wa Programu ya Mazingira na Michezo kwa Maendeleo, pamoja na vijana Yasin Juma na Salha Daniel. Kupitia mafunzo ya vitendo na kazi za vikundi, walijifunza mbinu mpya za kutumia michezo kama njia ya kuleta suluhisho kwa matatizo ya jamii.

Tunarudi nyumbani tukiwa na ujuzi mpya na tumejipanga kutumia yale tuliyojifunza ili kuendelea kuleta mabadiliko chanya kwa jamii kupitia michezo na ubunifu. 🕹️💡

YPM YAENDESHA SEMINA YA SIKU TATU MASHULENI KUHUSU UKATILI WA KIJINSIA (GBV)

Youth Peacemakers Tanzania (YPM) imeendesha semina ya siku tatu kwa wanafunzi wa shule tatu: Zingibari, Manza, na Kasera, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuelimisha vijana kuhusu madhara ya ukatili wa kijinsia (GBV) na jinsi ya kuutambua, kuuzuia, na kuripoti.

Katika semina hizi, wanafunzi walipata fursa ya kujifunza kwa kina kuhusu aina mbalimbali za ukatili wa kijinsia unaoweza kujitokeza majumbani, mashuleni, na kwenye jamii kwa ujumla. Pia walielimishwa juu ya haki zao, umuhimu wa kutoa taarifa pindi wanapokumbana na vitendo vya ukatili, na namna ya kujenga mazingira salama kwa wote.

Semina hizi zinalenga kuwajengea wanafunzi uelewa wa kutosha ili wawe mabalozi wa mabadiliko na walinzi wa haki za binadamu ndani ya jamii zao.

YPM inaendelea kujitolea katika kulinda haki za watoto na kuhimiza usalama, heshima, na utu kwa wote kupitia elimu ya kijamii.

YPM CONDUCTS THREE-DAY SCHOOL SEMINAR ON GENDER-BASED VIOLENCE (GBV)

Youth Peacemakers Tanzania (YPM) recently conducted a three-day seminar in three secondary schools: Zingibari, Manza, and Kasera, focusing exclusively on the topic of Gender-Based Violence (GBV).

During the sessions, students were equipped with in-depth knowledge about the different forms of GBV that may occur at home, in schools, and within the wider community. They also learned about their rights, the importance of speaking out, and how to report cases of violence safely and effectively.

The seminar aimed to raise awareness and empower students to become change-makers and protectors of human rights within their environments.

YPM remains committed to promoting safety, dignity, and justice for all through education and community engagement.

YPM Yaendesha Semina ya Ujasiriamali yenyelengo la Kuwajenga Vijana Na Akina Mama Vijana Uwezo wa kujitegemea Kiuchumi

Youth Peacemakers Tanzania (YPM) imeendesha semina ya ukombozi wa kiuchumi pamoja na masuala ya ukatili wa kijinsia ikiwa ni sehemu ya juhudi zake za kuwajengea uwezo vijana na akina mama vijana katika maeneo ya haki za kiuchumi, ulinzi wa mtoto na lishe kwaajili ya kudumisha amani endelevu.

Semina ya kwanza ilifanyika kwa siku mbili kuanzia tarehe 6-7 Mei 2025 na ililenga kuwapa vijana elimu juu ya haki za kiuchumi na kuwajengea uelewa wa masuala ya kijamii yanayowahusu, hususani umuhimu wa usawa wa fursa za kiuchumi katika jamii. Mafunzo haya yamewasaidia vijana kutambua nafasi yao katika kujiletea maendeleo na kushiriki kikamilifu katika shughuli za kijamii na kiuchumi.

Semina ya pili ilianza tarehe 8-9 Mei 2025 na ilikuwa maalum kwa ajili ya akina mama vijana. Mafunzo haya yaligusia kwa kina masuala ya ukatili wa kijinsia (GBV), malezi ya watoto, lishe bora, na haki za kiuchumi. Washiriki walipata nafasi ya kujifunza mbinu bora za kuwalea watoto wao, kulinda afya zao, na kujitambua kiuchumi ili waweze kujitegemea.

Kupitia semina hizi, YPM inaendelea kuunga mkono jitihada za kuleta mabadiliko chanya katika maisha ya vijana, kwa kuwapa maarifa na ujuzi muhimu kwa maendeleo yao binafsi na ya jamii zao.

YPM Conducts Economic Justice and GBV Seminars to Empower Youth and Young Mothers

Youth Peacemakers Tanzania (YPM) has successfully conducted economic justice and GBV seminars recently, as part of its ongoing efforts to empower young people and young mothers with knowledge on economic justice, child care, nutrition, and gender issues in Mkinga District.

The first seminar focused on equipping youth with essential knowledge on economic justice and raising their awareness on social issues that affect them. The training helped the youth understand their role in driving change and participating actively in economic and community development.

The second seminars, conducted over two days, were dedicated to young mothers. These sessions addressed key topics such as Gender-Based Violence (GBV), child care, proper nutrition, and economic justice. Participants were trained on how to better care for their children, improve their family health, and become economically independent.

Through these seminars, YPM continues to support the transformation of youth lives by offering relevant knowledge and practical skills to build better futures for themselves and their communities.