Bonanza la Vijana wa U13 na U20 Duga Maforoni

Bonanza la kuvutia lililoshirikisha jumla ya timu sita – mbili za U13 na nne za U20 – limefanyika katika viwanja vya Duga Maforoni.

Bonanza hili ni sehemu ya mradi wa pamoja kati ya CHRISC TANZANIA na YPM, likilenga kuwaandaa wataalamu wa michezo, hasa mpira wa miguu. Tayari hatua mbalimbali zimefanyika, ikiwemo:
✅ Kozi za makocha
✅ Mikutano ya wadau katika wilaya za Lushoto na Mkinga

Hadi sasa, makocha takribani 50 wameshiriki katika mafunzo haya, na matokeo yake yameanza kuonekana! Timu za vijana zimeanza kuundwa chini ya uongozi wa makocha hawa waliobobea.

Michezo ni msingi wa maendeleo ya vijana na jamii. Endelea kufuatilia kwa mengi zaidi kuhusu mradi huu.

#VijanaNaMichezo #CHRISC #YPM #U13 #U20 #SportsForDevelopment #MichezoKwaMaendeleo


U13 and U20 Youth Bonanza at Duga Maforoni
An exciting bonanza featuring six teams – two U13 and four U20 – took place at Duga Maforoni grounds.

This event is part of a joint project between CHRISC TANZANIA and YPM, aimed at developing sports experts, particularly in football. Key milestones achieved so far include:
✅ Coaching courses
✅ Stakeholder meetings in Lushoto and Mkinga districts

To date, approximately 50 coaches have participated in these trainings, and the results are already visible! Youth teams are now being formed under the leadership of these skilled coaches.

Sports are a cornerstone for youth and community development. Stay tuned for more updates on this impactful project.

#YouthInSports #CHRISC #YPM #U13 #U20 #SportsForDevelopment #YouthEmpowerment

Fainali ya Stop Poverty Cup Mkinga 2024

Timu ya Moa Stars imetawazwa kuwa mabingwa wa Stop Poverty Cup 2024 baada ya ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Kijiru Stars

Mashindano ya mwaka huu yaliendeshwa kwa kauli mbiu ya “4, 4, 2”, ikisisitiza umuhimu wa mikopo inayotolewa na serikali kupitia Halmashauri kwa WANAWAKE, VIJANA, na WALEMAVU. Lengo kuu ni kuhamasisha vijana kujiunga katika vikundi, kubuni miradi, na kuandaa maandiko bora ya miradi ili kufanikisha upatikanaji wa mikopo hiyo.

Vijana, huu ni wakati wako! Weka malengo, buni miradi, na chukua hatua kwa maendeleo ya jamii na kujitegemea kiuchumi.

#StopPovertyCup2024 #Mkinga #MikopoKwaVijana #MikopoKwaWanawake #MikopoKwaWalemavu #VijanaNaMaendeleo


Stop Poverty Cup Mkinga 2024 Finals
Moa Stars were crowned champions of the Stop Poverty Cup 2024 after a 3-0 victory against Kijiru Stars

This year’s tournament was held under the theme “4, 4, 2”, highlighting government loans provided through councils for WOMEN, YOUTH, and PEOPLE WITH DISABILITIES. The goal was to encourage young people to form groups, create innovative projects, and write solid project proposals to qualify for these loans.

Young people, this is your time! Set goals, develop projects, and take action toward community development and financial independence.

#StopPovertyCup2024 #Mkinga #LoansForYouth #LoansForWomen #LoansForPWDs #YouthEmpowerment

Mradi wa Miti na Elimu ya Mazingira kwa Vijana

Mradi wa miti unaosimamiwa na vijana katika eneo la Kanisa la Lutherani umepiga hatua kubwa, licha ya changamoto ya ukame na uhitaji wa mbegu zaidi lakini vijana wameonyesha juhudi kubwa. Meneja wa YPM Bw. Peter Jally amewashauri kuongeza uzito katika upandaji wa miti ya matunda, miti ya mbao, na hata maua, kwa kuwa pia ni biashara yenye faida.

Katika hatua nyingine, wanafunzi wa shule za msingi Maforoni A & B walipata elimu muhimu kuhusu Utetezi, Mazingira, na Michezo, wakiongozwa na maafisa wa YPM. Mafanikio zaidi yameonekana kwa kuanzishwa kwa kitalu cha miti ambacho sasa kinasubiri mbegu ili miti iweze kupandwa kwenye viriba vilivyokwishaandaliwa.

Katika shule ya sekondari Zingibari, elimu kuhusu masuala ya Utetezi, Mazingira, na Michezo ilitolewa pia. Wanafunzi wameahidi kuunda Peace Club, itakayofuatilia masuala kama mimba za utotoni na kuendesha kampeni nyingine zinazoendeshwa na YPM kwa shule na jamii kwa ujumla.

Hii ni hatua kubwa kuelekea maendeleo ya kijamii kupitia juhudi za pamoja za vijana, walimu, na YPM.

#UtunzajiWaMazingira #PeaceClubs #YPM #MazingiraNaVijana #MichezoKwaMaendeleo #MazaoNaBiashara


Youth-led Tree Planting and Environmental Education Project
A youth-led tree-planting project at the Lutheran Church grounds is making great progress despite challenges like drought and a need for more seeds, the youth have shown remarkable dedication. The Manager encouraged them to prioritize fruit and timber trees and to consider flowers as they are also a profitable venture.

Meanwhile, students from Maforoni A & B primary schools received vital education on Advocacy, Environment, and Sports, facilitated by YPM program officers. Notable progress includes the establishment of a tree nursery, which is now awaiting seeds to plant in already-prepared planting bags.

At Zingibari Secondary School, the same education was delivered, and students pledged to form a Peace Club. This club will focus on addressing issues like teenage pregnancies and running other campaigns initiated and supported by YPM within their school and the broader community.

These initiatives reflect a significant step toward community development through collaborative efforts of youth, teachers, and YPM.

#EnvironmentalCare #PeaceClubs #YPM #YouthForEnvironment #SportsForDevelopment #AdvocacyAndChange

Waratibu wa Ndani Watoa Maoni Muhimu Kuhusu Utafiti wa Maendeleo ya Vikundi vya SIGs

Youth Peacemakers Tanzania (YPM) imejumuisha waratibu wa ndani wa Vikundi vya Akiba na Mikopo ya Ndani (SIGs) ili kukusanya maoni kuhusu maendeleo na athari za vikundi hivyo. Hatua hii ni sehemu ya utafiti unaoendelea wa kutathmini ukuaji, ustahimilivu, na ufanisi wa SIGs katika kukuza uwezeshaji wa kiuchumi na uimara wa kijamii.

Waratibu walitoa maoni muhimu kuhusu mafanikio, changamoto, na fursa zilizopo ndani ya vikundi vyao. Maoni haya ni muhimu sana katika kusaidia YPM kuelewa hali halisi ya vikundi, na hivyo kuwezesha kubuni mikakati bora inayolingana na mahitaji ya wanachama wa SIGs.

Kupitia utafiti huu, YPM inalenga kuongeza athari chanya za SIGs kwa kushughulikia changamoto, kusherehekea mafanikio, na kuendeleza suluhisho bunifu kwa maendeleo endelevu.

Local Facilitators Provide Key Insights into SIGs Group Development Research

Youth Peacemakers Tanzania (YPM) has engaged local facilitators of Savings and Investment groups (SIGs) to gather feedback on the development and impact of these groups. This initiative is part of ongoing research aimed at evaluating the growth, sustainability, and effectiveness of SIGs in promoting economic empowerment and community resilience.

Facilitators shared valuable insights into the successes, challenges, and opportunities within their groups. These inputs are crucial in helping YPM understand the realities on the ground, enabling the organization to design more effective support strategies that align with the needs of SIGs members.

Through this research, YPM seeks to amplify the positive impact of SIGs by addressing challenges, celebrating successes, and fostering innovative solutions for sustained development.

YPM kwa Kushirikiana na CHRISC Yawawezesha Makocha na Walimu wa Michezo Kupitia Mafunzo ya Mpira wa Miguu

Youth Peacemakers Tanzania (YPM), kwa kushirikiana na CHRISC, imeendesha mafunzo ya kipekee kwa makocha wa mpira wa miguu na walimu wa michezo, yenye lengo la kuwawezesha kwa ujuzi na mbinu muhimu za kuendeleza michezo katika ngazi ya jamii.

Mafunzo haya yalihusisha mbinu za kisasa za ukufunzi, uongozi, na kukuza vipaji, yakiwajenga washiriki kuwa viongozi wa mabadiliko kwa vijana wanaojihusisha na michezo. Kupitia mafunzo haya, YPM na CHRISC zimedhihirisha dhamira yao ya kukuza maendeleo endelevu kupitia michezo.

Ushirikiano huu sio tu unajenga utaalamu bali pia unatoa fursa kwa vijana kung’ara katika michezo na maisha kwa ujumla. Hii inaonyesha dira ya pamoja ya kuimarisha mshikamano, afya, na uongozi kupitia programu za michezo ngazi ya jamii.

YPM and CHRISC Empower Coaches and Sports Teachers through Football Training

Youth Peacemakers Tanzania (YPM), in partnership with CHRISC, recently conducted an impactful training program aimed at equipping football coaches and sports teachers with essential skills and techniques to enhance sports development at the community level.

The training focused on advanced coaching methodologies, leadership, and talent nurturing, preparing participants to make a significant impact on young athletes. By bringing together passionate individuals dedicated to using sports as a tool for transformation, this initiative underscores the commitment of YPM and CHRISC to fostering sustainable development through sports.

This collaborative effort not only builds expertise but also creates opportunities for young people to thrive in sports and life. It reflects a shared vision to promote unity, health, and leadership through grassroots sports initiatives.

YPM na CHRISC Tanzania Waendesha Mafunzo ya Ualimu wa Michezo

Youth Peacemakers Tanzania (YPM), kwa kushirikiana na Christian Sports Contact Tanzania (CHRISC), wamezindua mpango wa mafunzo ya ualimu wa michezo unaolenga kuwawezesha walimu hao kua na mbinu bora za kimichezo.

Mafunzo haya yanawapa washiriki mbinu za kiufundi za kufundisha michezo, ujuzi wa uongozi, na maadili katika ualimu wa michezo. Kupitia michezo, programu inalenga kushughulikia changamoto za kijamii kama vile ukosefu wa ajira, usawa wa kijinsia, na migogoro ya kijamii.

Washiriki wanajumuisha walimu wa michezo wanaoanza na waliopo, viongozi wa vijana, na walimu wa shule kutoka maeneo mbalimbali. Mpango huu pia unahimiza ushiriki sawa wa wanawake na wanaume, ili kukuza usawa wa kijinsia katika michezo na uongozi.

Mafunzo haya ni sehemu ya maono ya YPM na CHRISC ya kujenga jamii zenye mshikamano na amani kupitia michezo, huku wakikuza uongozi na mshikamano miongoni mwa vijana. Ushirikiano huu unaonyesha dhamira yao ya pamoja ya kuwawezesha vijana na kubadilisha jamii kwa njia bunifu.

YPM and CHRISC Tanzania Conduct Sports Coaching Training

Youth Peacemakers Tanzania (YPM), in partnership with Christian Sports Contact Tanzania (CHRISC), has launched a dynamic sports coaching training program aimed at empowering coaches to become skilled sports coaches and leaders in their communities.

The training focuses on equipping participants with practical coaching techniques, leadership skills, and ethical approaches to sports. By integrating sports with community development, the program emphasizes using sports as a tool to address social challenges, such as unemployment, gender inequality, and conflicts.

Participants were existing coaches, teachers, and youth leaders. The initiative also prioritizes gender inclusivity, encouraging equal participation of men and women to foster equity in sports and leadership.

This training is part of YPM and CHRISC’s broader vision to build peaceful, cohesive communities through sports, cultivating leadership and teamwork among young people. The collaboration underscores their shared commitment to youth empowerment and social transformation through innovative approaches.

Mashine ya Shamba Kikundi cha “Lengo Letu” Yarejeshwa Kazi

Mashine ya shughuli za kilimo ya Kikundi cha “Lengo Letu” imefanyiwa marekebisho na sasa ipo tayari kutumika. Kwa marekebisho madogo yaliyosalia, kama kunoa visu, wanakikundi wamejitolea kuyakamilisha kwa kushirikiana.

Mashine hii inawawezesha wakulima kwenda sambamba na mabadiliko ya teknolojia kama hatua muhimu kuelekea kilimo cha kisasa. Lengo ni kufanikisha kilimo chenye tija kinacholeta faida kwa wakulima huku kikizingatia utunzaji wa mazingira.

Katika hatua nyingine, semina ya ujasiriamali kuhusu ufugaji wa kuku iliandaliwa kwa wanachama wa vikundi vya VICOBA. Semina hiyo ilifanyika katika ofisi ya Kikundi cha VICOBA cha “Lengo Letu” huko Kijiru, Kata ya Mayomboni. Madhumuni yalikuwa kuwapa wanajamii maarifa ya kujitegemea kiuchumi na kuongeza kipato kwa kuzingatia mbinu bora za ufugaji.

Tunalenga kuimarisha vikundi kupitia elimu na nyenzo bora kwa maendeleo endelevu ya kiuchumi na kijamii.

#VICOBA #LengoLetu #Ujasiriamali #UfugajiWaKuku #KilimoBora #MaendeleoEndelevu

Lengo Letu Group’s Farm Machine Restored
The agricultural machine of the “Lengo Letu” group has been repaired and is now ready for use. Minor fixes, such as blade sharpening, will be completed by the group members themselves through teamwork.

This machine enables the farmers to embrace technological advancements as a crucial step toward modern farming. The goal is to achieve productive agriculture that benefits the farmers while promoting environmental conservation.

In another development, an entrepreneurship seminar on poultry farming was conducted for members of VICOBA groups. The seminar took place at the office of the “Lengo Letu” VICOBA group in Kijiru, Mayomboni Ward. The objective was to equip the community with skills for economic self-reliance and to boost incomes by adopting effective poultry farming practices.

Our mission remains to strengthen groups through education and practical tools for sustainable economic and social development.

#VICOBA #LengoLetu #Entrepreneurship #PoultryFarming #ModernFarming #SustainableDevelopment

Uzinduzi wa Mafunzo ya Football Coaching

Imekuwa wiki ya mafanikio makubwa kwa YPM, kwani mafunzo ya football coaching yameanza kwa kishindo na ushiriki wa washiriki wengi zaidi ya matarajio. Lengo la mafunzo haya ni kuwajengea walimu na wakufunzi wa mpira wa miguu ujuzi na maarifa ya kisasa ili kuimarisha kiwango cha michezo katika jamii zetu. Mafanikio haya yanaonesha ari na shauku ya washiriki katika kukuza vipaji na kuleta mabadiliko chanya kupitia michezo.

Mafunzo haya yanatoa fursa kwa washiriki kujifunza mbinu za kisasa za ufundishaji, usimamizi wa timu, na jinsi ya kuwajenga wachezaji kiakili na kimwili ili kufikia viwango vya juu zaidi. Washiriki wamefurahia mafunzo ya leo, na wengi wameeleza kuridhishwa na ubora wa maudhui na walimu wanaoendesha mafunzo haya.

Tunashukuru kwa mwitikio huu mkubwa na tunawashukuru wote waliohusika kufanikisha maandalizi haya. Mafunzo yameendeshwa kwa siku mbili zaidi, na tunatarajia kuona ufanisi zaidi kadri washiriki wanavyoendelea kupata maarifa.

It has been a Week of great success for YPM, as the football coaching training program officially kicked off with an overwhelming number of participants, exceeding initial expectations. The goal of this training is to equip coaches and football instructors with modern skills and knowledge to enhance the level of sports in our communities. This success demonstrates the enthusiasm and commitment of participants to develop talent and bring positive change through sports.

The training provides participants with valuable insights into modern coaching techniques, team management, and strategies to support players both mentally and physically to achieve higher performance levels. Many attendees expressed satisfaction with the quality of the content and the expertise of the trainers leading the sessions.

We are grateful for the impressive turnout and extend our appreciation to everyone involved in organizing this event. The training has been conducted for two days, and we look forward to seeing more success as participants continue to gain knowledge.

Youth Peacemakers Tanzania katika Maonesho ya Usambara Marathon Festival Wilayani Lushoto

Mkuu wa Mkoa Mh. Batilda Buriani akimvisha medali ya ushindi Moses Kazula mwakilishi kutoka taasisi ya YPM, baada ya kuibuka kuwa mshindi wa kwanza katika mbio za km5.

Wafanyakazi wa Youth Peacemakers Tanzania (YPM) walishiriki kwenye maonesho ya Usambara Marathon Festival yaliyofanyika katika viwanja vya Nyerere Square, wilayani Lushoto. Maonesho hayo yalivutia idadi kubwa ya washiriki na wadau, yakiwa na lengo la kuhamasisha afya kupitia michezo na kuleta pamoja jamii kwa ajili ya kujifunza na kubadilishana mawazo kuhusu maendeleo ya jamii.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mheshimiwa Batilda Buriani, alihudhuria na kuongoza maonesho hayo, ambapo alipata fursa ya kuona jitihada mbalimbali zinazofanywa na mashirika kama YPM katika kuhamasisha maendeleo ya vijana na jamii kupitia michezo na shughuli nyingine za kijamii.

YPM ilitumia fursa hii kuonyesha kazi yao ya kipekee katika kuendeleza vijana kupitia mipango ya maendeleo endelevu kama vile uhamasishaji wa amani, mazingira, na michezo kwa maendeleo. Maonyesho haya yameonyesha kwa mara nyingine umuhimu wa ushirikiano kati ya wadau wa michezo na mashirika ya kijamii katika kujenga taifa lenye afya na lenye mafanikio.

Youth Peacemakers Tanzania inaendelea kuwa mstari wa mbele katika kuleta mabadiliko chanya kwa jamii kupitia mipango yake ya kijamii na maendeleo.

Maadhimisho ya Miaka 10 ya Youth Peacemakers Tanzania

Safari ya Mafanikio na Maendeleo

Agosti 31, 2024 – Lushoto, Tanga                                              

Youth Peacemakers Tanzania (YPM) imetimiza miaka 10 ya uwepo wake kwa mafanikio makubwa na sherehe za kuvutia zilizofanyika katika viwanja vya Nyerere Square, Lushoto, Tanga. Tukio hili muhimu lilileta pamoja wanavikundi vya VICOBA, wanafunzi wa Peace Clubs, wawezeshaji wa miradi, pamoja na mgeni rasmi, Mhe. Mwanaidi Ali Khamis, ambaye alitoa hotuba yenye hamasa na kupongeza juhudi za YPM katika kujenga jamii yenye amani na maendeleo.

Maadhimisho haya yalikuwa fursa ya kipekee ya kuangalia safari ya miaka kumi iliyopita, ambayo imejaa changamoto na mafanikio. Mkutano ulianza kwa neno la ukaribisho kutoka kwa Mkurugenzi Mwanzilishi wa YPM, Mchungaji Godfrey Tahona Walalaze, ambaye aliwakumbusha washiriki juu ya maono yaliyoweka msingi wa kuanzishwa kwa YPM: kuwajengea uwezo vijana wa Kitanzania kuwa viongozi wa amani na maendeleo katika jamii zao.

Mhe. Mwanaidi Ali Khamis alitoa hotuba yenye hamasa, akipongeza juhudi za YPM katika kuwawezesha vijana kupitia miradi mbalimbali kama VICOBA na Peace Clubs. Alisisitiza umuhimu wa kuendelea kushirikiana na YPM katika kuboresha maisha ya vijana na jamii kwa ujumla.

Huku tukisherehekea mafanikio ya miaka kumi, YPM inajiandaa kwa miaka mingine kumi ya huduma na maendeleo. Tumepanga kuendelea kuimarisha na kupanua programu zetu ili kuwafikia vijana wengi zaidi na kuleta mabadiliko chanya katika jamii za Kitanzania. Tutaendelea kushirikiana na wadau wetu, kuhakikisha tunajenga jamii yenye amani, usawa, na maendeleo endelevu.

YPMT inatoa shukrani za dhati kwa washirika, wafadhili wa shughuli (NMB, TIGO na CRDB), , na jamii tunazozitumikia kwa kutuunga mkono katika safari hii. Mafanikio yetu yamejengwa juu ya msingi wa ushirikiano wenu, na kwa pamoja tutaendelea kuleta mabadiliko katika jamii zetu.

Tunatarajia kuona mafanikio zaidi katika miaka ijayo. Endelea kufuatilia habari na taarifa zetu kupitia tovuti na mitandao yetu ya kijamii ili kuona jinsi unavyoweza kushiriki katika kazi zetu.

Youth Peacemakers Tanzania 10th Anniversary Celebration:

A Journey of Success and Growth

August 31, 2024 – Lushoto, Tanga

Youth Peacemakers Tanzania (YPM) celebrated its 10th anniversary with a remarkable event held at Nyerere Square in Lushoto, Tanga. This significant milestone brought together VICOBA group members, Peace Clubs students, project facilitators, and the Guest of Honor, Hon. Mwanaidi Ali Khamis, who delivered an inspiring speech praising YPM’s efforts in building peaceful and prosperous communities.

This anniversary provided a unique opportunity to reflect on the past ten years a journey filled with challenges and achievements. The event commenced with a welcoming address by YPM’s Founding Director, Mchungaji Godfrey Tahona Walalaze, who reminded attendees of the vision that laid the foundation for YPM: to empower Tanzanian youth to become leaders of peace and development within their communities.

Hon. Mwanaidi Ali Khamis delivered a motivating speech, commending YPM’s efforts in empowering youth through various initiatives such as VICOBA and Peace Clubs. She emphasized the importance of continued collaboration with YPM to improve the lives of youth and the broader community.

As we celebrate a decade of success, YPM is preparing for the next ten years of service and development. We plan to continue strengthening and expanding our programs to reach more youth and bring positive change to Tanzanian communities. We will continue to collaborate with our partners to build peaceful, equitable, and sustainable communities.

We would like to express our heartfelt gratitude to our partners, donors (NMB, TIGO, and CRDB), and the communities we serve for supporting us on this journey. Our success has been built on the foundation of your cooperation, and together we will continue to make a difference in our communities.

We look forward to more achievements in the coming years. Stay connected with us through our website and social media platforms to follow our journey and see how you can get involved in our work.