Blue Economy Seminar

Semina ya uchumi wa bluu.

Leo vijana wa YPM pamoja na vijana wa mradi wa change wamepata nafasi ya kushiriki semina ya uchumi wa bluu na kujifunza kuhusu ufugaji wa samaki na fursa zilizopo kwenye ufugaji wa samaki nyumbani kwa kijana mjasiriamali ambae pia ni kijana wa kujitolea katika ofisi za YPM. Kijana Yasini Juma ameanzisha bwawa la samaki ambapo anafuga samaki aina ya sato.

Yasini aliwaeleza kuwa wazo la biashara ndio kitu kikubwa pamoja na kulitumikia wazo hilo ili kuleta matokeo chanya. Alizidi kusisitiza kwamba vijana wanapaswa kujiamini na kutilia maanani kile wanacho kifanya ili waweze kufanikiwa.

Blue economy seminar.

Today YPM youth as well as the youth of the change project have had the opportunity to hold a blue economy seminar to learn about fishing and the opportunities in the aquaculture industry, at home of a young entrepreneur who is also a volunteer in YPM offices. Yasini Juma has set up a fish pond where he raises sato fish. Yasini has explained to them that the idea of a business is a big thing as well as serving this idea to bring about positive results.

He further emphasized that young people should be confident and considerate of what they are doing in order to be successful.

Health Education Training

Health Education Training

Washiriki wa Mradi wa Change wakiwa na vijana wengine wakati wa mafunzo ya Elimu ya Afya na Makuzi ya vijana yaliongozwa na Mtaalamu wa Afya kutoka katika Hospitali ya Wilaya Hai (Boma) Dr. Glory Kimario ambae pia ni kijana wa kujitolea katika ofisi za Youth Peacemakers hapa Lushoto. Dhumuni la mafunzo hayo nikuwawezesha vijana kuongeza uwelewa juu ya afya zao na kujua jinsi gani wanaweza kukabiliana na changamoto za kifya ili pia waweze kuwasaidia wengine katika jamii zao kutatua changamoto hizo.

Change participants during the training

Taifa imara linategemea vijana hivyo imara kwa vijana ndio nguvu ya maendeleo.

Mafunzo ya Elimu ya Afya.

Participants during the training

Change Project Participants with other young people during the Health Education and Youth Growth Development training led by a Health Specialist from Hai District Hospital (Boma) Dr. Glory Kimario who is also a young volunteer at the Youth Peacemakers offices here in Lushoto. The purpose of the training is to enable young people to raise awareness about their health and to know how to cope with health challenges so that they can also help others in their community to solve these. challenges.

Dr. Glory Kimario facilitating

The power of a nation depends on the power of the young people.

Welcome Our Partners from Norway

Welcoming our partners from Y-Global to YPM.

We are very pleased to welcome you to the YPM and we hope you will have a nice stay here in Lushoto.

Karibuni wageni wetu kutoka Norway.

Rev. Godfrey Walalaze at the middle speaking to the guests from Norway

Tunafurahi sana kuwakaribisha Lushoto na ni matumaini yetu mtafurahia.

Debate

This Friday Shambalai Secondary School had a Debate with Mombo Secondary School on the topic ” Science and Techonology have brought more harm than good in third world countries”

We are happy that young people had managed to argue and share their thoughts about the topic.

International Celebration of Women’s Day

Maazimisho ya siku ya wanawake duniani.

Kila tarehe 8 ya mwezi Machi dunia inasheherekea siku ya wanawake duniani. Katika ngazi ya Wilaya YPM imeungana na maasifa wa serikali wakiongozwa na mgeni rasmi ambae ni Mkuu wa Wilaya Lushoto Mheshimiwa Karisti Lazaro, Mkurgenzi mtendanji mheshimiwa Ikupa Mwaisyoge pamoja na maafisa wengine. Maadhimisho hayo yalikua na kaulimbiu isemayo ”Usawa wa kijinsia wa leo,kesho na endelevu”.Sio hivyo tu bali wanachi na wanafunzi walijitokeza kwa wingi kusheherekea siku hiyo.

World Women’s Day celebrations.

Every March 8th the world celebrates International Women’s Day. At the district level YPM is joined by government officials led by the official guest who is Lushoto District Commissioner Hon. Karisti Lazaro, Executive Director Hon. Ikupa Mwaisyoge and other officials. The theme of commemoration was “Gender equality today, tomorrow and sustainability”. Not only that but citizens and students turned out in large numbers to celebrate the day.

Young Person who managed to save the World

Young Person who managed to save the world.

It is from YPM Peace Club to the Environment Champion.

Meet Leonard Antony Msumari who completed his O-level studies in 2021 at Prince Claus Secondary School in Lushoto district. Leonard is 19 years old and lives with his parents in the village of Irente which is about two and a half miles from where he lives. When he started his studies in 2018 he joined the YPM Peace club which has been established by the YPM Tanzania Organisation for the purpose of mobilizing young people on environmental stewardship. While working with the YPM Peace club, Mr. Antony expressed admiration for the way the club grew up caring for the environment by organizing tree nurseries and planting trees. Leonard not only actively participated in the club activities and showed his ability and high motivation in the club, but also took the distributed trees and planted them in their fields. However, Mr. Antony became more interested in setting up a nursery at his home place. Speaking to YPM staff, Mr. Antony said that he has so far sold 36000 trees to the community members and planted a total of 1500 trees from last year to now. YPM staff are pleased to see young people actively involved in liberating the world and find the solution for tackling the issue of climate change. Congratulations to Mr. Leonard Antony on this milestone and we are behind him to support him in this movement. Our call to the youth is to support the efforts of rescuing the world from the challenges which are being brought by climate change.

Kijana aliefanikiwa kuikoa dunia.

Ni kutoka YPM klabu ya Amani mpaka mpigania haki za mazingira.

Kutana na Leonarld Antony Msumari ambae ni  ni mwanafunzi aliehitimu masomo yake ya kidato cha nne mwaka 2021 katika  Shule ya Secondari Prince Claus Hapa wilayani Lushoto. Leonard ana umri wa mika 19 na anaishi na wazazi wake katika kijiji cha Irente ambapo ni kilometa takribani mbili na nusu kutoka nyumbani anapoishi. Wakati alipoaanza masomo yake mwaka 2018 alijiunga na YPM Peace club ambayo imeanzishwa na taasissi ya YPM Tanzania kwa lego la kuwahamasisha vijana juu ya utunzaji wa mazingira. Alipokua kwenye YPM Peace club ndugu Leonard alionyesha kufurahishwa na jinsi club hiyo ilivyokua inatunza mazingira kwa kuandaa vitalu vya miti na kupanda miti. Leonard alishiriki kikamilifu lakini pia hakuishia kuonyesha uwezo wake na hamasa ya juu shuleni tu, bali alichukua miti waliogaiwa nakuipanda kwenye mashamba yao. Hata hivyo ndugu Leonard alivutiwa zaidi na akaanzisha kitalu cha miti nyumbani kwao. Akizungumza na wafanyakazi wa YPM ndugu antony amesema kwamba mpaka sasa ameuza miti 36,000 na amepanda jumla ya miti 1500 toka mwaka jana hadi sasa. Uongozi wa YPM umefurahishwa sana kuona vijana wanashiriki kikamilifu katika kuiokoa dunia na mabadiliko ya hali ya hewa. Tunampongeza sana ndugu Leonard kwa hatua hii aliofikia nakwamba tupo nyuma yake kumuunga mkono katika harakati hizi.Wito wetu kwa vijana nikuwaomba kuunga jitihanda zinazofanywa na dunia ilikuiokoa kutoka kwenye janga la mabadiliko ya hali ya hewa.

Take Charge for Our Future

Mabadiliko ya tabianchi ni changamoto kubwa inayosumbua dunia. Hii nikutokana na kuambatana na majanga makubwa Kama vile ukame au mafuriko ambayo huhatarisha maisha ya mwanadamu hapa duniani. Katika jitihada za kupambana na changamoto hii, Ubalozi wa uholanzi nchini Tanzania uliandaa mkutano uliokutanisha takribani vijana 100 kutoka sehemu mbalimbali katika jengo la taasisi ya Alliance Françise jini Dar es salaam kwa lengo la kuwahamasisha vijana kuchukua jukumu la kuyalinda mazingira kwa vitendo  ilikuifanya dunia kuwa sehemu salama kuishi.

Mkutano ulifunguliwa na salamu za ukaribisho kutoka kwa balozi wa Uholanzi nchini Tanzania na wazungumzaji rasmi walikua ni vijana wanaharakati wa kutetea mazingira na kila mmoja alieleza hadithi yake ambayo Ilikua na mguso wa namna yake tangu alipoanza harakati hadi aliposasa. Hadithi zao zilikua hamasa kubwa kwelikweli kiasi cha kumfanya kila kijana akiwa na ari ya kutaka kupanda miti Kama sehemu ya kuyalinda na kuyatunza mazingira.

Katika kipindi cha maswali na majibu ilibainika kuwa shauku ya kutaka kupunguza mabadiliko ya tabia ya nchi ni kubwa sana kuliko matendo yanayofanyika, hii nikutokana na kuwa na sera nzuri na elimu pia, lakini changamoto yake ni kwamba havimpi ulazima mwanamchi kulibeba jukumu la kuyalinda mazingira.

Makubaliano ni kwamba changamoto hii iendelee kuzungumzwa kukuza uelewa wa raia lakini lazima zitafutwe mbinu zitakazomlazimisha kila mmoja kutunza mazingira ama akiwa anataka au hataki kwakuwa hata katika familia unaweza kuandaa chakula kizuri kinachoweza kumfanya mtoto awe na afya tele lakini yeye akakataa kula. Hivyo lazima itafutwe mbinu alazimishwe kula ilianufaike na chakula kile. Vinginevyo mikutano ya namna hii itakosa nguvu kwanza itakuwa ikijadili tu na kuandaa mikakati mizuri lakini utekelezaji hakuna na changamoto itabaki palepale.

Kutoka Taasisi ya Vijana Waleta Amani Tanzania vijana 13 walipata nafasi ya kushiriki mkutano huo. Mbali na kukuza uelewa na hamasa kutoka kwa vijana wenzao walipata wasaa mzuri wa kutengeneza marafiki wapya kutoka taasisi mbalimbali zilizo hudhuria hivyo kuifanya familia ya Vijana Waleta Amani kutambulika na kuwa kubwa zaidi.

Climate change is a major challenge facing the world. This is due to the presence of major disasters such as droughts or floods that endanger human life on earth. In an effort to address this challenge, the Dutch Embassy in Tanzania organized a conference that brought together about 100 young people from various parts of the Alliance Françise building in Dar es Salaam with the aim of motivating young people to take responsibility for environmental protection to make the world a better place to live.

The meeting was opened with welcome greetings from the Dutch Ambassador to Tanzania and the official speakers were young activists and each told his own story which was very inspiring and have its kind of impact from the beginning to the present. Their stories very impressive that they made every young person want to plant trees as part of protecting and caring for the environment.

During the question-and-answer session it was found that the desire to reduce climate change is far greater than the actions taking place, this is due to having good policies and education as well, but the challenge is that they do not give citizens the responsibility to protect the environment.

The consensus is that this challenge should continue to be discussed to raise public awareness but strategies must be employed that will force everyone to take care of the environment whether they want it or not because even in the family you can prepare healthy food that can keep a child healthy but he or she refuses to eat. So a method must be employed to force him to eat in order to benefit from that food. Otherwise meetings of this nature will lack strength first will only discuss and devise good strategies but no implementation and challenges will remain the same.

From the YPM Tanzania 13 young people had the opportunity to participate in the conference. In addition to nurturing understanding and motivation from their peers, they also had the opportunity to make new friends from various attending Organization, thus making the YPM family big recognizable.

Global Disability Summit

Mkutano wa kimataifa wa walemavu.

Tarehe 14 Feb – 17Feb Norway na Ghana waliandaa mkutano wa kimataifa wakishirikina na Uingereza juu ya watu wenye ulemavu Duniani. Mkutano huu ulifanyika kwa njia ya mtandao ambapo watu mbalimbali waliwezakushiriki wakiwa majumbani kwao. Ilikua imetarajiwa kwamba watuwangeweza kukaa pamoja na kushiriki wakiwa wanaonana laikini kulingana na changamoto zilizosababishwa na ungojwa wa Korona basi ukapelekea mkutano huu kufanyika kwa njia ya mtandao. Hata hivyo hii haikupunguza maana ya Mkutano huo kwani yote yaliopangwa kujadiliwa yalijadiliwa hususa ikiwa ni kutengeneza mazingira mazuri katika nyanja mbalimbali ilikuwawezesha watu wenye mahitaji maalumu kutumia fursa izo. Mmoja wa washiriki alisikika akisema kua ” Watu wenye ulemavu wanaweza kusoma na kuelewa vizuri kama wanafunzi wengine endapo watawekewa mazingira mazuri ya  kujifunzia” na hili linaenda sambamba hata katika nyanja nyingine mfano kwenye ajira watu wenye ulemavu wanapaswa kupewa nafasi na kuwekewa mazingira mazuri ya kuwawezesha wao kufanya kazi bila kikwazo chochote.

Katika siku hizi zote za mkutano YPM iliweza kuandaa vijana wapatao kumi na moja  ambao kunawalioshiriki wakiwa ndani ya ofisi za YPM wakati wengine wakishiriki wakiwa majumbani mwao.

Global Disability Summit.

On 14 Feb – 17 Feb Norway and Ghana hosted an international conference in partnership with the United Kingdom on Persons with Disabilities in the World. The meeting was held online where various people were able to participate in their homes. It was hoped that the people would be able to sit down and participate and see each other but depending on the challenges posed by COVID-19 Pandemic then it led to the conference being held online. However, this did not diminish the meaning of the Conference as all that was planned such as creating a conducive environment in various fields which will enable people with special needs to interact, work or study without any obstacle. One of the participants was heard to say that “People with disabilities can learn and understand like other students if they are provided with a good learning environment” and this goes hand in hand even in other areas such as employment to help people with disability to work without any hindrance.

During all the days of the conference YPM was able to organize about 11 young people who participated in the YPM offices while others were participating from their homes.

Merry Christmas and Happy New Year 2022

Mpendwa rafiki na mshirika wa YPM, ninamshukuru Mungu kwa ajili yako kwa kupewa neema ya kufikia majira haya ya Krismasi. Ni mwaka unakamilika sio kwa nguvu zetu bali kwa huruma yake Mungu.

Ninawapongeza kwa kujituma katika majukumu mbalimbali, pamoja na changamoto ya Korona au Uviko 19 iliyoendelea mwaka 2021, bado tumeweza kushirikiana na kutimiza majukumu yetu. Ninawapa pole wale ambao waliugua, waliopoteza ndugu na kwa njia moja au nyingine waliopoteza hata mali zao katika kuhangaikia kuponya Maisha yao na ndugu zao. Kwenu wote ninapenda kusema Hongera kwa utayari, kujituma na kupambana hata kufikia siku ya leo.

Ni matumaini yangu kuwa tunapouelekea mwaka 2022 tutaendelea kusimama pamoja, kuwa na nia moja na kujitoa kwa ajili ya kutekekeleza majukumu yetu ya taaasisi.

Kwa washirika wetu – Y global na wengineo, wafanyakazi wenzangu, marafiki wa ndani na nje na kipekee watendakazi pamoja nasi katika ngazi za serikali na wananchi mmoja mmoja

Ninawatakia Sikukuu njema ya Krismasi na Heri kwa mwaka mpya wa 2022.

Amani ya Bwana Mungu iwe nanyi siku zote.

Dear friend and partner of YPM, I thank God for you for being given the grace to reach this Christmas season. It is a year that ends not by our own strength but by God’s mercy.

I commend you for your commitment to the various roles, despite the challenge of COVID-19 which continued in 2021, we have still been able to co-operate and fulfil our responsibilities. I offer my condolences to those who became ill, lost loved ones and in one way or another lost even their possessions in the pursuit of healing their Lives and their loved ones. To all of you I would like to say Congratulations on your readiness, dedication and fighting to this day.

It is my hope that as we move towards 2022 we will continue to stand together, be united and committed to fulfilling our organisation mission.

To our partners – Y global and others, my colleagues, friends inside and outside Tanzania and in unique way to the colleagues with us in government as well as fellow citizens,

I wish you a Merry Christmas and a Happy New Year 2022.

May the peace of the Lord God be with you always.

Rev. Godfrey T. Walalaze

Director YPM Tanzania.