The Mkinga Stop Poverty Cup

Taasisi ya YPM imeendelea kuendesha mashindano ya Mkinga Stop Poverty Cup Football league yanayofanyika kila mwaka katika Wilaya ya Mkinga Mkoani Tanga. Mashindano haya yameleta manufaa makubwa sana katika jamii ya watu wa Mkinga kama alivyozungumza Diwani wa Kata ya Moa, “Naishukuru Taasisi ya Youth Peace Makers Tanzania kwakutuletea mashindano haya ambayo yamewafanya vijana kujihusisha kikamilifu katika shughuli za michezo na maendeleo na kupunguza vitendo vya wizi mtaani”.

YPM inafurahi kuona kwamba malengo ya kuanzisha mashindano haya ya mpira wa miguu yanafikiwa hususani kuwakomboa vijana kutoka katika wimbi la umasikini kwa kutumia vipaji vyao ilikujipatia kipato. Pamoja na hayo mashindao haya yalianzishwa ili kutokomeza vitendo vya kigaidi na kuwafanya vijana wajitambue na kukataa kutumiwa na watu wenye nia mbaya ya kuchafua amani.

Ikumbukwe Wilaya Mkinga ni moja ya Wilaya zilizopo mpakani na mara kadha kumekua kukiripotiwa uwepo wa makundi na watu wageni wenye nia mbaya yakutaka kuvuruga amani. Tunashukuru kwamba kupitia mashindano haya vijana wameweza kujitambua na kutambua nafasi zao katika jamii. Tunapenda kutoa pongezi kwa vikundi vya PeaceMakers vinavyotoa huduma ndogo za fedha katika jamii vya Kijiru na Karoyo (Comunity Microfinance Groups) ambavyo vimeshirikiana na kuandaa mashindano haya. Pia tunashukuru vijana wote, wazee na viongozi wa serikali walioshiriki katika mashindano haya.

YPM has continued to run the Mkinga Stop Poverty Cup Football league which is usually held annually at Mkinga District in Tanga Region. The competition has brought great benefits to the Mkinga community, as Moa ward Councilor said “I thank the Youth Peace Makers Tanzania orgaisation for bringing us this competition, this competition has made young people actively involved in sports and development activities and reduce acts of violence and street theft “.

YPM is pleased to see that the goals of establishing this football tournament are being achieved in particular to liberate young people from the chains of poverty by using their talents to generate income. However, the competition was launched to eradicate terrorism and to make young people aware of and refuse to be manipulated by people with malicious intent to disturb the peace.

It should be noted that, Mkinga District is one of the border districts and there have been several reports of groups and foreigners with malicious intent to disrupt the peace. We are grateful that through this competition young people have been able to identify themselves and realize their place in society.

We would like to congratulate the Peacemakers groups of Kijiru and Karoyo who provide financial services to the communities (Community Microfinance Groups) and had collaborated and organized this competition. We also thank all the young people, the elderly and government officials who participated in this competition.