YPM na CHRISC Tanzania Waendesha Mafunzo ya Ualimu wa Michezo

Youth Peacemakers Tanzania (YPM), kwa kushirikiana na Christian Sports Contact Tanzania (CHRISC), wamezindua mpango wa mafunzo ya ualimu wa michezo unaolenga kuwawezesha walimu hao kua na mbinu bora za kimichezo.

Mafunzo haya yanawapa washiriki mbinu za kiufundi za kufundisha michezo, ujuzi wa uongozi, na maadili katika ualimu wa michezo. Kupitia michezo, programu inalenga kushughulikia changamoto za kijamii kama vile ukosefu wa ajira, usawa wa kijinsia, na migogoro ya kijamii.

Washiriki wanajumuisha walimu wa michezo wanaoanza na waliopo, viongozi wa vijana, na walimu wa shule kutoka maeneo mbalimbali. Mpango huu pia unahimiza ushiriki sawa wa wanawake na wanaume, ili kukuza usawa wa kijinsia katika michezo na uongozi.

Mafunzo haya ni sehemu ya maono ya YPM na CHRISC ya kujenga jamii zenye mshikamano na amani kupitia michezo, huku wakikuza uongozi na mshikamano miongoni mwa vijana. Ushirikiano huu unaonyesha dhamira yao ya pamoja ya kuwawezesha vijana na kubadilisha jamii kwa njia bunifu.

YPM and CHRISC Tanzania Conduct Sports Coaching Training

Youth Peacemakers Tanzania (YPM), in partnership with Christian Sports Contact Tanzania (CHRISC), has launched a dynamic sports coaching training program aimed at empowering coaches to become skilled sports coaches and leaders in their communities.

The training focuses on equipping participants with practical coaching techniques, leadership skills, and ethical approaches to sports. By integrating sports with community development, the program emphasizes using sports as a tool to address social challenges, such as unemployment, gender inequality, and conflicts.

Participants were existing coaches, teachers, and youth leaders. The initiative also prioritizes gender inclusivity, encouraging equal participation of men and women to foster equity in sports and leadership.

This training is part of YPM and CHRISC’s broader vision to build peaceful, cohesive communities through sports, cultivating leadership and teamwork among young people. The collaboration underscores their shared commitment to youth empowerment and social transformation through innovative approaches.

Mashine ya Shamba Kikundi cha “Lengo Letu” Yarejeshwa Kazi

Mashine ya shughuli za kilimo ya Kikundi cha “Lengo Letu” imefanyiwa marekebisho na sasa ipo tayari kutumika. Kwa marekebisho madogo yaliyosalia, kama kunoa visu, wanakikundi wamejitolea kuyakamilisha kwa kushirikiana.

Mashine hii inawawezesha wakulima kwenda sambamba na mabadiliko ya teknolojia kama hatua muhimu kuelekea kilimo cha kisasa. Lengo ni kufanikisha kilimo chenye tija kinacholeta faida kwa wakulima huku kikizingatia utunzaji wa mazingira.

Katika hatua nyingine, semina ya ujasiriamali kuhusu ufugaji wa kuku iliandaliwa kwa wanachama wa vikundi vya VICOBA. Semina hiyo ilifanyika katika ofisi ya Kikundi cha VICOBA cha “Lengo Letu” huko Kijiru, Kata ya Mayomboni. Madhumuni yalikuwa kuwapa wanajamii maarifa ya kujitegemea kiuchumi na kuongeza kipato kwa kuzingatia mbinu bora za ufugaji.

Tunalenga kuimarisha vikundi kupitia elimu na nyenzo bora kwa maendeleo endelevu ya kiuchumi na kijamii.

#VICOBA #LengoLetu #Ujasiriamali #UfugajiWaKuku #KilimoBora #MaendeleoEndelevu

Lengo Letu Group’s Farm Machine Restored
The agricultural machine of the “Lengo Letu” group has been repaired and is now ready for use. Minor fixes, such as blade sharpening, will be completed by the group members themselves through teamwork.

This machine enables the farmers to embrace technological advancements as a crucial step toward modern farming. The goal is to achieve productive agriculture that benefits the farmers while promoting environmental conservation.

In another development, an entrepreneurship seminar on poultry farming was conducted for members of VICOBA groups. The seminar took place at the office of the “Lengo Letu” VICOBA group in Kijiru, Mayomboni Ward. The objective was to equip the community with skills for economic self-reliance and to boost incomes by adopting effective poultry farming practices.

Our mission remains to strengthen groups through education and practical tools for sustainable economic and social development.

#VICOBA #LengoLetu #Entrepreneurship #PoultryFarming #ModernFarming #SustainableDevelopment

Uzinduzi wa Mafunzo ya Football Coaching

Imekuwa wiki ya mafanikio makubwa kwa YPM, kwani mafunzo ya football coaching yameanza kwa kishindo na ushiriki wa washiriki wengi zaidi ya matarajio. Lengo la mafunzo haya ni kuwajengea walimu na wakufunzi wa mpira wa miguu ujuzi na maarifa ya kisasa ili kuimarisha kiwango cha michezo katika jamii zetu. Mafanikio haya yanaonesha ari na shauku ya washiriki katika kukuza vipaji na kuleta mabadiliko chanya kupitia michezo.

Mafunzo haya yanatoa fursa kwa washiriki kujifunza mbinu za kisasa za ufundishaji, usimamizi wa timu, na jinsi ya kuwajenga wachezaji kiakili na kimwili ili kufikia viwango vya juu zaidi. Washiriki wamefurahia mafunzo ya leo, na wengi wameeleza kuridhishwa na ubora wa maudhui na walimu wanaoendesha mafunzo haya.

Tunashukuru kwa mwitikio huu mkubwa na tunawashukuru wote waliohusika kufanikisha maandalizi haya. Mafunzo yameendeshwa kwa siku mbili zaidi, na tunatarajia kuona ufanisi zaidi kadri washiriki wanavyoendelea kupata maarifa.

It has been a Week of great success for YPM, as the football coaching training program officially kicked off with an overwhelming number of participants, exceeding initial expectations. The goal of this training is to equip coaches and football instructors with modern skills and knowledge to enhance the level of sports in our communities. This success demonstrates the enthusiasm and commitment of participants to develop talent and bring positive change through sports.

The training provides participants with valuable insights into modern coaching techniques, team management, and strategies to support players both mentally and physically to achieve higher performance levels. Many attendees expressed satisfaction with the quality of the content and the expertise of the trainers leading the sessions.

We are grateful for the impressive turnout and extend our appreciation to everyone involved in organizing this event. The training has been conducted for two days, and we look forward to seeing more success as participants continue to gain knowledge.

Youth Peacemakers Tanzania katika Maonesho ya Usambara Marathon Festival Wilayani Lushoto

Mkuu wa Mkoa Mh. Batilda Buriani akimvisha medali ya ushindi Moses Kazula mwakilishi kutoka taasisi ya YPM, baada ya kuibuka kuwa mshindi wa kwanza katika mbio za km5.

Wafanyakazi wa Youth Peacemakers Tanzania (YPM) walishiriki kwenye maonesho ya Usambara Marathon Festival yaliyofanyika katika viwanja vya Nyerere Square, wilayani Lushoto. Maonesho hayo yalivutia idadi kubwa ya washiriki na wadau, yakiwa na lengo la kuhamasisha afya kupitia michezo na kuleta pamoja jamii kwa ajili ya kujifunza na kubadilishana mawazo kuhusu maendeleo ya jamii.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mheshimiwa Batilda Buriani, alihudhuria na kuongoza maonesho hayo, ambapo alipata fursa ya kuona jitihada mbalimbali zinazofanywa na mashirika kama YPM katika kuhamasisha maendeleo ya vijana na jamii kupitia michezo na shughuli nyingine za kijamii.

YPM ilitumia fursa hii kuonyesha kazi yao ya kipekee katika kuendeleza vijana kupitia mipango ya maendeleo endelevu kama vile uhamasishaji wa amani, mazingira, na michezo kwa maendeleo. Maonyesho haya yameonyesha kwa mara nyingine umuhimu wa ushirikiano kati ya wadau wa michezo na mashirika ya kijamii katika kujenga taifa lenye afya na lenye mafanikio.

Youth Peacemakers Tanzania inaendelea kuwa mstari wa mbele katika kuleta mabadiliko chanya kwa jamii kupitia mipango yake ya kijamii na maendeleo.

Maadhimisho ya Miaka 10 ya Youth Peacemakers Tanzania

Safari ya Mafanikio na Maendeleo

Agosti 31, 2024 – Lushoto, Tanga                                              

Youth Peacemakers Tanzania (YPM) imetimiza miaka 10 ya uwepo wake kwa mafanikio makubwa na sherehe za kuvutia zilizofanyika katika viwanja vya Nyerere Square, Lushoto, Tanga. Tukio hili muhimu lilileta pamoja wanavikundi vya VICOBA, wanafunzi wa Peace Clubs, wawezeshaji wa miradi, pamoja na mgeni rasmi, Mhe. Mwanaidi Ali Khamis, ambaye alitoa hotuba yenye hamasa na kupongeza juhudi za YPM katika kujenga jamii yenye amani na maendeleo.

Maadhimisho haya yalikuwa fursa ya kipekee ya kuangalia safari ya miaka kumi iliyopita, ambayo imejaa changamoto na mafanikio. Mkutano ulianza kwa neno la ukaribisho kutoka kwa Mkurugenzi Mwanzilishi wa YPM, Mchungaji Godfrey Tahona Walalaze, ambaye aliwakumbusha washiriki juu ya maono yaliyoweka msingi wa kuanzishwa kwa YPM: kuwajengea uwezo vijana wa Kitanzania kuwa viongozi wa amani na maendeleo katika jamii zao.

Mhe. Mwanaidi Ali Khamis alitoa hotuba yenye hamasa, akipongeza juhudi za YPM katika kuwawezesha vijana kupitia miradi mbalimbali kama VICOBA na Peace Clubs. Alisisitiza umuhimu wa kuendelea kushirikiana na YPM katika kuboresha maisha ya vijana na jamii kwa ujumla.

Huku tukisherehekea mafanikio ya miaka kumi, YPM inajiandaa kwa miaka mingine kumi ya huduma na maendeleo. Tumepanga kuendelea kuimarisha na kupanua programu zetu ili kuwafikia vijana wengi zaidi na kuleta mabadiliko chanya katika jamii za Kitanzania. Tutaendelea kushirikiana na wadau wetu, kuhakikisha tunajenga jamii yenye amani, usawa, na maendeleo endelevu.

YPMT inatoa shukrani za dhati kwa washirika, wafadhili wa shughuli (NMB, TIGO na CRDB), , na jamii tunazozitumikia kwa kutuunga mkono katika safari hii. Mafanikio yetu yamejengwa juu ya msingi wa ushirikiano wenu, na kwa pamoja tutaendelea kuleta mabadiliko katika jamii zetu.

Tunatarajia kuona mafanikio zaidi katika miaka ijayo. Endelea kufuatilia habari na taarifa zetu kupitia tovuti na mitandao yetu ya kijamii ili kuona jinsi unavyoweza kushiriki katika kazi zetu.

Youth Peacemakers Tanzania 10th Anniversary Celebration:

A Journey of Success and Growth

August 31, 2024 – Lushoto, Tanga

Youth Peacemakers Tanzania (YPM) celebrated its 10th anniversary with a remarkable event held at Nyerere Square in Lushoto, Tanga. This significant milestone brought together VICOBA group members, Peace Clubs students, project facilitators, and the Guest of Honor, Hon. Mwanaidi Ali Khamis, who delivered an inspiring speech praising YPM’s efforts in building peaceful and prosperous communities.

This anniversary provided a unique opportunity to reflect on the past ten years a journey filled with challenges and achievements. The event commenced with a welcoming address by YPM’s Founding Director, Mchungaji Godfrey Tahona Walalaze, who reminded attendees of the vision that laid the foundation for YPM: to empower Tanzanian youth to become leaders of peace and development within their communities.

Hon. Mwanaidi Ali Khamis delivered a motivating speech, commending YPM’s efforts in empowering youth through various initiatives such as VICOBA and Peace Clubs. She emphasized the importance of continued collaboration with YPM to improve the lives of youth and the broader community.

As we celebrate a decade of success, YPM is preparing for the next ten years of service and development. We plan to continue strengthening and expanding our programs to reach more youth and bring positive change to Tanzanian communities. We will continue to collaborate with our partners to build peaceful, equitable, and sustainable communities.

We would like to express our heartfelt gratitude to our partners, donors (NMB, TIGO, and CRDB), and the communities we serve for supporting us on this journey. Our success has been built on the foundation of your cooperation, and together we will continue to make a difference in our communities.

We look forward to more achievements in the coming years. Stay connected with us through our website and social media platforms to follow our journey and see how you can get involved in our work.

Ufuatiliaji wa vikundi vidogo vya kijamii vya huduma ndogo za Kifedha (SIGS) na Mpango wa Elimu ya Mazingira

Katika juhudi za kina za kutathmini athari zake kwa muongo mmoja uliopita, Youth Peacemakers Tanzania (YPM) imefanya ufuatiliaji wa wiki mbili na makundi ya vikundi vidogo vya kijamii vya huduma ndogo za kifedha (SIGS) ambavyo vinasimamiwa na taasisi. Mpango huu unalenga kutathmini mafanikio na changamoto zinazokabiliwa na makundi haya, kubaini idadi ya vikundi hivyo ambavyo bado vinafanya kazi, na kupima utiifu wao katika ufuatiliaji wa sheria zinazoongoza vikundi hivyo.

Maafisa wa YPM walitembelea maeneo kadhaa yenye vikundi hivyo vya huduma ndogo za kifedha, ikiwemo Mgombezi Korogwe, Konje Handeni, Handeni Mjini, Maili Kumi Handeni, Kwamasimba Korogwe, Kijiru, Kichalikani, na Duga Maforoni huko Mkinga. Makundi haya ya vikundi vidogo vya kijamii vya huduma ndogo za fedha (SIGS) yameonyesha utaratibu mzuri na utiifu wa kufuata sheria zilizowekwa na serikali pamoja na katiba za vikundi vyenyewe, hali iliyochangia mafanikio yao ya kudumu.

Mbali na ufuatiliaji na vikundi hivyo YPM imechukua hatua za kukuza uhamasishaji wa mazingira kwa kutoa semina  kwa walimu wa mazingira wa shule za msingi na sekondari za Wilayani Mkinga, zikilenga kuhimiza kampeni za mazingira miongoni mwa wanafunzi. Maafisa pia walitembelea kituo cha mafunzo ya Kompyuta kilichopo Tanga mjini na Wilaya ya Mkinga, vijiji vya Azimio na Tanganyika ili kutambulisha programu za YPM na kutoa ufahamu juu ya dhamira na malengo yake kwa ujumla.

Monitoring and evaluation of small investment groups (SIGS) and Environmental Education Initiatives

In a comprehensive effort to evaluate its impact over the past decade, Youth Peacemakers Tanzania (YPM) has conducted a two-week follow-up with small investments groups (SIGs) managed by the organization. This initiative aims to assess the successes and challenges faced by these groups, determine the number of active SIGs, and measure their adherence to the governing laws and regulations.

YPM officers visited several locations with these Small investments groups, including Mgombezi Korogwe, Konje Handeni, Handeni Mjini, Maili Kumi Handeni, Kwamasimba Korogwe, Kijiru, Kichalikani, and Duga Maforoni in Mkinga. These small investments groups (SIGs) have demonstrated strong organization and adherence to the laws established by the government and the groups’ constitutions, contributing to their sustained success.

In addition to the follow-up with these groups, YPM has taken steps to promote environmental awareness by providing seminars to primary and secondary school environmental teachers in Mkinga District. These seminars aim to encourage environmental campaigns among students. The officers also visited the computer center in Tanga city and Mkinga district, villages of Azimio and Tanganyika to introduce YPM’s programs and provide insights into its overall mission and objectives.

Ufuatiliaji wa Matumizi ya Rasilimali za Umma

Mkutano wa Asasi zinazosimamia Ufuatiliaji wa Matumizi ya Rasilimali za Umma

Youth Peacemakers Tanzania imejumuika na asasi mbalimbali za kiraia zinazosimamia utekelezaji wa mfumo wa ufuatiliaji wa matumizi ya rasilimali za umma nchini Tanzania.


Mkutano huo umefanyika kwa njia ya mtandao kupitia mtandao wa Zoom, ukijumuisha zaidi ya asasi 153 katika kujadili namna ya kupata muongozo mmoja utakaosimamia mfumo huo wa ufuatiliaji wa matumizi ya rasilimali za umma.
Mfumo wa ufuatiliaji wa matumizi ya rasilimali za umma ni mfumo unaowekwa na serikali au taasisi husika ili kufuatilia na kudhibiti jinsi rasilimali za umma zinavyotumika. Lengo kuu la mfumo huu ni kuhakikisha uwajibikaji, uwazi, na ufanisi katika matumizi ya fedha za umma.

Mkataba wa Makubaliano Kati ya YPM Tanzania na CHAMAVITA

Youth Peacemakers Tanzania (YPM) na CHAMAVITA wamesaini makubaliano ya ushirikiano wenye lengo la kuhamasisha amani na maendeleo ya jamii nchini Tanzania. Ushirikiano huu utatumia nguvu za mashirika yote mawili ili kukuza utatuzi wa migogoro, kuwawezesha vijana, na kuanzisha miradi ya maendeleo endelevu kote nchini.

YPM Tanzania, inayojulikana kwa juhudi zake za msingi katika ujenzi wa amani na ushirikishaji wa vijana, itafanya kazi kwa karibu na CHAMAVITA, shirika lililo na dhamira ya maendeleo ya jamii na mshikamano wa kijamii, kutekeleza programu na miradi ya pamoja. Programu hizi zitajumuisha warsha za elimu ya amani, mazungumzo ya jamii, na mafunzo ya ujenzi wa uwezo kwa viongozi vijana.

Ushirikiano kati ya mashirika haya mawili unatarajiwa kuwa na athari kubwa kwa jamii za mitaa kwa kuchanganya rasilimali na utaalamu, YPM Tanzania na CHAMAVITA wanakusudia kushughulikia mizizi ya migogoro na kuunda jamii jumuishi na yenye amani zaidi.

Juhudi za pamoja pia zitalenga kuwawezesha vijana kuwa mawakala wa mabadiliko, wakiwa na ujuzi na maarifa yanayohitajika kuongoza juhudi za ujenzi wa amani katika jamii zao. Ushirikiano huu unaonyesha umuhimu wa ushirikiano katika kufanikisha amani na maendeleo endelevu, na mashirika yote mawili yana matumaini kuhusu matokeo chanya yatakayopatikana.

Memorandum of Understanding between YPM Tanzania CHAMAVITA

Youth Peacemakers Tanzania (YPM) and CHAMAVITA have signed an agreement for the collaboration aimed at fostering peace and community development in Tanzania. The partnership will leverage the strengths of both organizations to promote conflict resolution, youth empowerment, and sustainable development initiatives across the country.

YPM Tanzania, known for its grassroots efforts in peace building and youth engagement, will work closely with CHAMAVITA, an organization dedicated to community development and social cohesion, to implement joint programs and initiatives. These programs will include peace education workshops, community dialogues, and capacity-building training for young leaders.

The collaboration between the two organizations is expected to have a significant impact on local communities by combining resources and expertise, YPM Tanzania and CHAMAVITA aim to address the root causes of conflict and create a more inclusive and peaceful society.

The joint efforts will also focus on empowering young people to become agents of change, equipping them with the skills and knowledge needed to lead peace building efforts in their communities. This partnership underscores the importance of collaboration in achieving sustainable peace and development, and both organizations are optimistic about the positive outcomes it will bring.

Environmetal Management Act Review

Environmental Management Act

Youth Peacemakers brought together young people from the Institute of Judicial Administration (IJA), YPM Youth Forum in Moshi who have come from Machame and KCMC health colleges, along with other participants from Iringa health University and Prince Claus Secondary School in Lushoto. These young people had the opportunity to jointly review the Environmental Management Act of 2024 and reconcile the following matters; –

i/ The law is strong in managing the environment

ii/ It has been seen that society still does not understand enough about this law

iii/ There is no effective management of this law in our areas. After analysing this, the young people agreed on two things to work on in the region of Tanga and Kilimanjaro where the first thing is to provide education on the rights and responsibilities of every citizen on environmental care but also to motivate and cooperate with the Government to ensure that this law it is implemented in our communities.

Sheria ya Usimamizi wa Mazingira

Youth Peacemakers iliwaleta kwa pamoja vijana kutoka Chuo cha Uongozi wa Mahakama (IJA), YPM Youth Forum ya Moshi ambao wametoka Vyuo vya afya vya Machame na KCMC,pamoja  na  washiriki wengine waliooka Chuo cha afya cha Iringa na shule ya Sekondari ya  Prince Claus  iliopo Lushoto. Vijana hawa walipata nafasi ya kupitia kwa pamoja Sheria ya Usimamizi wa Mazingira ya mwaka 2024 na kuanisha mambo yafuatayo; –

i/ Sheria ipo imara katika kusimamia mazingira

ii/ Imeonekana jamii bado hainauwelewa wakutosha juu ya sheria hii

iii/Hakuna usimamizi madhubuti wa sheria hii katiaka maeneo yetu.

Baada ya kuchambua haya vijana hao walikubaliana mambo mawili ya kufanyia kazi katika mkoa wa Tanga na Kilimanjaro ambapo jambo la kwanza ni kuotoa elimu juu ya haki na wajibu wa kila raia juu ya utunzaji wa mazingira lakini pia kuhamasiha na kushirikia na Serikali ili kuhakikisha kwamba sheria hii inatekelezwa na kufuatwa katika jamii zetu.