Maadhimisho Siku ya Mtoto wa Afrika

Mtoto wa Afrika: Imarisha Ulinzi na Fursa Sawa kwa Watoto

Youth Peacemakers Tanzania (YPM) kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto, wameungana pamoja katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika yaliyofanyika Kiwilaya katika kata ya Dule, jimbo la Mlalo, tarehe 16 juni 2024.

Mtoto wa Afrika ni maadhimisho yanayofanyika kila mwaka tarehe 16 Juni, kwa lengo la kuwakumbuka watoto wa kitongoji cha Soweto nchini Afrika ya Kusini waliouawa tarehe 16 Juni, 1976 kutokana na uwepo wa ubaguzi wa rangi.

Katika harakati za kudai haki zao za kutobaguliwa pamoja na haki nyingine za kibinadamu kama elimu bora kwa watoto wote, watoto hao waliuliwa kikatili, hivyo mnamo mwaka 1990 Umoja wa Nchi Huru za Afrika (OAU) kwa sasa (AU), walipitisha Azimio la kuwakumbuka watoto hao waliokua na uthubutu wa kupigania haki zao.

Kauli mbiu ya mwaka huu ni “Maendeleo Endelevu 2030: Imarisha Ulinzi na Fursa Sawa kwa Watoto” ikiwa na lengo la kuwakumbusha wazazi, walezi, Serikali na wadau wengine kuzingatia wajibu wetu katika kuimarisha mifumo ya ulinzi na maendeleo ya Mtoto ili aweze kudhibiti changamoto ya ongezeko la vitendo vya ukatili nchini pamoja na kutoa haki sawa kwa watoto wote bila ubaguzi wa aina yoyote.

Child of Africa: Strengthen Protection and Equal Opportunities for Children

Youth Peacemakers Tanzania (YPM), in collaboration with the Lushoto District Council, have joined together in the celebration of the International  African Child day held at the district level at Dule ward, in Mlalo constituency, on June 16, 2024.

International African Child day is an annual commemoration held on June 16, aiming to remember the children of Soweto, South Africa, who were killed on June 16, 1976, due to the existence of racial segregation.

In their struggle to demand their rights against discrimination, as well as other human rights such as quality education for all children, these children were brutally killed. Hence, in 1990, the Organization of African Unity (OAU), now the African Union (AU), passed a resolution to remember these brave children who fought for their rights.

This year’s theme is “Sustainable Development 2030: Strengthen Protection and Equal Opportunities for Children,” with the aim of reminding parents, guardians, the government, and other stakeholders to fulfill our duty in strengthening child protection systems and development. This is to address the increasing challenges of violence against children in the country and to ensure equal rights for all children without any form of discrimination

Kipindi cha Redio kuelekea Siku ya Mtoto wa Afrika

Mjadala Maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika

Kuelekea siku ya maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika Youth Peacemakers Tanzania, wameratibu mjadala wa kuielimisha jamii juu ya maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika, kwa kuwaalika vijana wanaounda Peace clubs kutoka Chuo cha uongozi wa mahakama IJA pamoja na wanafunzi wa shule za sekondari katika studio za redio ya Utume FM.

Mjadala huo wenye lengo la kuibua changamoto zinazowakabili watoto, ikiwemo unyanyasaji, ndoa za utotoni, mimba za utotoni na ukatili dhidi ya watoto, umelengwa kuikumbusha jamii kutopuuzia au kukaa kimya pindi wanapoona haki za mtoto zinakiukwa.

Jamii ikishirikiana na serikali katika kuibua vitendo viovu vinavyowakumba watoto, itasaidia utekelezaji wa sera ya maendeleo endelevu ya mwaka 2030, yenye lengo la kuhakikisha kila mtoto anapata haki na wajibu stahiki.

Discussion on the Commemoration of the Intenational African Child Day

As we approach the commemoration of the International African Child Day, Youth Peacemakers Tanzania has organized a discussion to educate the community about this important day. They have invited youth from Peace Clubs at the Judicial Leadership Institute (IJA) and students from secondary schools to participate in the discussion at the studios of Utume FM radio.

This discussion aims to highlight the challenges facing children, including abuse, child marriages, teenage pregnancies, and violence against children. The goal is to remind the community not to ignore or remain silent when they witness violations of children’s rights.

By collaborating with the government to expose the evil acts affecting children, the community can contribute to the implementation of the Sustainable Development Goals for 2030, which aim to ensure that every child receives the appropriate rights and responsibilities.

Youth Peacemakers Whistle-Blowing Policy

Whistle-blower Policy

Fraud and corruption diverts resources from the poor. It breaches the ethics and values of YPM, damages the reputation for sound financial management, and further damages the reputation in public and in relation to partners. Corruption has come to be recognized as one of the greatest obstacles to development. The YPM policy on fraud and corruption is one of zero tolerance. We strive to be transparent in all our work and believe that openness is fundamental in the fight against corruption and other kinds of unethical behaviour. To ensure that our policies are put into practice we urge anyone who suspects corruption or other violations of our policy to notify us. In the form below you can report any incidents, or suspicion of incidents, of corruption, bribery, other business crime, harassment of any kind, or unacceptable behaviour. You will always have the option of staying anonymous when reporting an incident. Nevertheless, we do encourage you to provide your name and contact information in the report, as it makes it easier for us to follow up on your complaint. Your report and identity will always be treated confidentially.

WHO CAN COMPLAIN?

  1. Anyone affected by our work or by projects we support has a right to complain.
  2. Our partners, volunteers, and staff.
  3. Donors and other YPM stakeholders

WHAT TO COMPLAIN ABOUT?

  • Suspicion of or witness of inappropriate behaviour or misconduct by a YPM staff or Board member, a volunteer, or by someone representing one of our partners.
  • Sexual, physical, verbal, or psychological harassment.
  • Suspicion of misuse of funds/fraud.

YPM WILL NOT CONSIDER AND HANDLE COMPLAINTS THAT ARE:

  • Found to be malicious accusations intended to serve personal objectives and agendas.
  • Intended to generate unnecessary bureaucracy and administration by reporting issues already discussed and decided on in line with proper procedures.
  • Complaints that are already the subject of legal proceedings.

HOW WILL A COMPLAINT TO YPM BE HANDLED?

In case of suspected fraud or corruption reported by staff, volunteers, or third parties to YPM, the YPM Board of Directors will have the responsibility to delegate the case to the correct special committee who will follow up on the case. The board committee will assess the allegation(s) and consider whether to launch an investigation. Feedback on whether the incident will be investigated further will be given within fourteen working days of the submission of the complaint. If an investigation with appropriate parties is established, the concerned party will be taken out on forced leave during the investigation. After concluding the case, the follow-up will meet the laws in the country where the incident has taken place. There will be extra emphasis on securing the safety of the person who has brought the concern to YPM.

CONTACT INFORMATION FOR COMPLAINTS:

If you do not wish to use the online complaint form (below), you can contact the YPM Director or the Chair of the YPM Board directly. If the complaint is about the Director, please contact the Chairperson of the Board.

Rev. Godfrey T. Walalaze, The Director

Telephone: (+255) 7865 364 489 // E-mail: director@youthpeacemakers.or.tz/ godfrey.walalze@peacemakers.no

Rev. John Sembuyagi, Chairperson of the Board

Telephone: (+255) 784 552 541 // E-mail:sembuyag@gmail.com 

Below is a link to the online complaint form

https://forms.office.com/r/ft2YF1ax4e

Reflection on YPM’S WORK

Siku zimepita,miezi ikapita miaka nayo ikapita na hata majira yamebadilika. Sio hivyo tu bali hata walikokua wakitwa vijana kipindi hicho inawezekana kwa sasa sio vijana tena. Haya yote yanatupa kufikiria tulikotoka mpaka tulipo sasa. Kama mdau wa YPM unapoana picha kama hizi unakumbuka nini?

Days have passed, months have passed and years have passed and even the seasons have changed. Not only that, but even those who used to be called young people during that period are probably not young anymore. All this gives us a chance to reflect about where we came from to where we are now. As a YPM stakeholder, what do you remember when you see the below pictures?

#Tafakuriyamiaka10yaYPM

GBV training

Norec exchange participant hosted a two-day GBV training with volunteers from YPM who were passionate about learning and eager to join the community to raise awareness!

SIGs Monitoring and Evaluation

Ufuatiliaji wa Vikundi vya Kijamii vya Huduma Ndogo za Kifedha .

YPM imeendela kutembelea na kutatua changamoto mbambali ambazo Vikundi vya Kijamii vya Huduma Ndogo za Kifedha vinakumbaza nazo hasa katika swala zima la uwendeshaji wa vikundi hivi. awamu hii YPM imepata nafasi ya kutembelea vikundi vya Mbumbuli Msongolo na Funta.

Monitoring of Microfinance Social Groups.

YPM has continued to visit and solve the various challenges that Community Microfinance Groups are facing, especially in the whole issue of the operation of these groups. In this phase YPM has had the opportunity to visit the groups of Bumbuli Msongolo and Funta.

Young Facilitator Training

Mafunzo ya wawezeshaji Vijana

Tarehe 18 na 19 Desemba 2023 YPM iliendesha mafunzo ya wawezeshaji vijana wa Vikundi vya Kijamii vya Huduma Ndogo za Fedha kutoka maeneo ya Malibwi, Bumbuli, Ngulwi, Korogwe , Makanya na Magamba. Kama taasisi inayojihusisha na maendeleo ya vijana ilikuomboa jamii, YPM imeweka mkazo katika kuwawezesha vijana hawa ili waweze kuwawezesha wengine katika uwanzishaji na usimamizi wa vikundi hivi, ili sheria, kanuni na taratibu zilizoweka na Serikali ya Jamhuri ya Muugano wa Tanzania zifuate ilikuleta maendeleo endelevu katika jamii.

Young SIGs Facilitators training

On the 18th and 19th of December 2023 YPM conducted the training of young facilitators of the Community Microfinance Groups (CMGs) from the areas of Malibwi, Bumbuli, Ngulwi, Korogwe, Makanya and Magamba. As an organisation that is involved in the development of young people in the community, YPM has focused on empowering these young people so that they can empower others in the establishment and management of these groups, so that the laws, regulations and procedures set by the Government of the United Republic of Tanzania are followed to bring sustainable development in the community.

Youth Change Summit (YCS)2023

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Khamis Hamza Khamis amewakumbusha vijana wenye uelewa kuhusu mazingira kutoa elimu hiyo kwa wananchi wa vijijini wasio na uelewa juu ya athari za uharibifu wa mazingira  ili kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.

Amesema hayo katika ufunguzi wa Kongamano la vijana la Youth Change Summit linalojadili mada mbalimbali za mabadiliko ya tabia nchi lililo fanyika  kwa siku mbili wilayani Moshi Mkoa wa Kilimanjaro, ambapo amesema ni wakati wa vijana wasomi kuipeleka elimu hiyo maeneo ambayo hayafikiki kirahisi ili kujenga uelewa juu ya athari na madhara yatokanayo na uharibifu wa mazingira.

Participants of YCS 2023

Katika hotuba yake pia Mh.Khamis amesema Serikali kupitia Ofisi ya Makamu wa Rais inatekeleza miradi mbalimbali ikiwemo kuwezesha upatikanaji wa majiko banifu ambayo yanasaidia kupunguza au kuondosha kabisa vitendo vya ukataji miti kwa ajili ya kuni na mkaa sambamba na kuhamasisha matumizi ya mkaa mbadala.

Katika hatua nyingine amebainisha Serikali inaendelea na utaratibu wa kupunguza Kodi Katika nishati mbadala ili wananchi waweze kustahimili kwa kila kaya.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa taasisi ya Youth PeaceMakeres Tanzania Mch. Godfrey Tahona Walalaze amesema wamelenga kufanya Kongamano hili la Mazingira kwa kulenga Mabadiliko ya tabia Nchi kwakuwa linaathiri maisha ya binadamu kwa ujumla  na wakiamini vijana wanauwezo mzuri wa kubuni njia bora za kukabiliana na chanzo na athari ya Mabadiliko ya Tabia Nchi kwa maisha ya Sasa na baadae.